Back to Learning Plans

Mkombozi: Mafunzo yenye Athari Kubwa Kutoka Surah Al-Mulk

Mkombozi: Mafunzo yenye Athari Kubwa Kutoka Surah Al-Mulk
Duration:
Each short Lesson takes less than 10 minutes to complete 7 Lessons total.
Description:

Safari hii ya siku 7 ndani ya Surah Al-Mulk inakualika kutembea aya kwa aya ndani ya moja ya surah zenye uzito mkubwa katika Qur’ani, Surah ambayo Mtume (Rehema na amani zimshukie) aliielezea kuwa ni yenye kumuombea msomaji wake mpaka asamehewe.

Mtume Muhammad (Rehema na amani zimshukie) pia aliisema kuwa:
“هي المنجية من عذاب القبر”
(Jami‘ at-Tirmidhi 2890)
Yaani: “Hii ndiyo inayomkomboa (msomaji wake) na adhabu ya kaburi.”

Katika kipindi cha juma moja, utaweza kushuhudia Ufalme wa Allah, kusudi la maisha na kifo, ukamilifu wa uumbaji, uhalisia wa Akhera, na utegemezi wako wa kila siku kwa Allah.

Mwisho wa safari hii, hutaelewa tu mada kuu za Surah Al-Mulk, bali utahisi kusukumwa na aya zake — kuibadilisha hekima kuwa yakini, na yakini kuwa vitendo, inshaAllah.

Mada Zinazojadiliwa 

  • Utawala kamili wa Allah juu ya uumbaji wote

  • Kusudi la maisha na kifo

  • Ishara za ukamilifu wa Allah katika uumbaji

  • Uhakika wa Jahannamu na Jannah

  • Ikhlasi na ibada za siri

  • Shukrani kwa neema za kila siku

  • Mafunzo kutoka kwa mataifa yaliyopita

Anza leo, ili uchukue hatua moja kuelekea karibu na moyo uliotiwa nanga kwa imani.

Wasiliana nasi kupitia: [email protected] 

About the author:
  • Timu ya QuranReflect Mpango huu wa kujifunza umetayarishwa na Timu ya QuranReflect ili kuwasaidia wanaojifunza kuhusiana na Qur'ani kwa njia iliyo na mpangilio na yenye manufaa kwa maisha ya kila siku. Maudhui yameundwa ili yawe yenye maana na thabiti katika uelewa sahihi, yakihimiza tafakari na kuimarisha muunganiko wa kina na Qur'ani katika kila hatua.