Mwenyezi Mungu Alipowaruzuku, yule mume na mke, mtoto mwema walimfanyia Mwenyezi Mungu washirika katika mtoto yule ambaye Mwenyezi Mungu Alipwekeka katika kumuumba wakamfanya ni mja wa asiyekuwa Mwenyezi Mungu; Ametukukuka Mwenyezi Mungu na Ameepukana na kila mshirika.