Watawajibu kwa kusema, «Ndio! Tumejiwa na Mjumbe anayetoka kwa Mwenyezi mungu akatuonya na tukamkanusha na tukasema kuhusu miujiza aliyokuja nayo: Mwenyezi Mungu hakumteremshia binadamu kitu chochote. Hamkuwa nyinyi, enyi Mitume, isipokuwa mmeenda mbali na haki.