«Ama wale waliomkanusha al- Masīḥ miongoni mwa Mayahudi, au wakamzidishia sifa miongoni mwa Wanaswara, nitawaadhibu adhabu kali katika ulimwengu: kwa kuuawa, kunyang’anywa mali na kuondolewa ufalme, na katika Akhera kwa Moto; na hawatakuwa na msaidizi mwenye kuwanusuru na kuwaepushia adhabu ya Mwenyezi Mungu.»