Akakaa hud-hud muda usio mrefu kisha akahudhuria, na Sulaymān akamlaumu juu ya kughibu kwake na kutokuwako kwake. Hud-hud akamwambia, «Nimejua jambo usilolijuwa kikamilifu, na nimekujia kutoka mji wa Saba’ na habari ya jambo muhimu sana, na mimi nina yakina nalo.