Na waja wa Mwingi wa rehema walio wema ni wale ambao wanatembea juu ya ardhi kwa utulivu wakiwa wanyenyekevu; na wajinga mafidhuli wanaposema nao maneno ya kuwaudhi wanawapa majibu mazuri na wanasema nao maneno ya kuwafanya wasalimike na dhambi na (pia wasalimike na) kukabiliana na mjinga kwa ujinga wake.